Mpya

Libasse amemaliza adhabu CAF, Kapombe bado - Ahmed

Mwana Msimbazi By Mwana Msimbazi
β€’
9 Sep 2026
Libasse amemaliza adhabu CAF, Kapombe bado - Ahmed

Klabu ya Simba imethibitisha kuwa kiungo wake, Libasse Geye, amemaliza adhabu yake ya kadi nyekundu katika mashindano ya CAF na anaruhusiwa kurejea kwenye kikosi kitakachokutana na Mighty Wanderers katika mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Akizungumza, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amesema Libasse alimaliza adhabu yake baada ya kukosa mechi mbili za Ligi ya Mabingwa Afrika, huku beki Shomari Kapombe akiwa bado anapaswa kutumikia adhabu yake.

Libasse alionyeshwa kadi nyekundu baada ya mchezo dhidi ya Petro de Luanda uliochezwa Februari 7, 2026 nchini Angola na kumalizika kwa sare ya bao 1-1. Ahmed amesema tukio hilo lilitokea baada ya mchezo kumalizika, tofauti na Kapombe ambaye alitolewa wakati mchezo ukiendelea.

Kwa mujibu wa Ahmed, tukio lililosababisha kadi hiyo lilihusisha pia mchezaji wa Simba, Alassane Kante, lakini waamuzi walimchukulia hatua Libasse.

Kutokana na adhabu hiyo, Libasse alikosa michezo miwili ya Ligi ya Mabingwa Afrika; dhidi ya Stade Malien katika msimu wa 2025/26 na dhidi ya Mighty Wanderers katika hatua ya kwanza ya msimu wa 2026/27.

Hivyo, kurejea kwa Libasse kunampa Simba chaguo jingine muhimu katika eneo la kiungo wakati timu hiyo ikijiandaa kwa mchezo wa marudiano dhidi ya Mighty Wanderers.

Kwa upande mwingine, Kapombe ambaye pia ni majeruhi, bado hajaimaliza adhabu yake ya kukosa mechi tatu, hivyo atawakosa Mighyty Wonderers

More Stories

Karibu Azam Complex kwenye show za Libasse Gueye
Karibu Azam Complex kwenye show za Libasse Gueye
29m ago
READ MORE β†’
Mzizima Derby; Azam Fc vs Simba leo
Mzizima Derby; Azam Fc vs Simba leo
3h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Jumatano, Septemba 16 2026
Magazeti ya leo Jumatano, Septemba 16 2026
6h ago
READ MORE β†’
Maandalizi ya kuikabili Azam Fc yamekamlika
Maandalizi ya kuikabili Azam Fc yamekamlika
15h ago
READ MORE β†’
Hatuhitaji kupoteza mchezo dhidi ya Azam Fc - Barker
Hatuhitaji kupoteza mchezo dhidi ya Azam Fc - Barker
1d ago
READ MORE β†’
Mzizima Derby haijawahi kuwa nyepesi
Mzizima Derby haijawahi kuwa nyepesi
1d ago
READ MORE β†’
Kituo kinachofuata ni MZIZIMA DERBY
Kituo kinachofuata ni MZIZIMA DERBY
1d ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Jumanne, Septemba 15 2026
Magazeti ya leo Jumanne, Septemba 15 2026
1d ago
READ MORE β†’
Doumbia bado kidogo, Mgunda akosha mashabiki
Doumbia bado kidogo, Mgunda akosha mashabiki
1d ago
READ MORE β†’
Tulitaka kutuma ujumbe Afrika - Ahmed
Tulitaka kutuma ujumbe Afrika - Ahmed
1d ago
READ MORE β†’