Mpya

Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo

Mwana Msimbazi By Mwana Msimbazi
β€’
1d ago
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo

Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Clatous Chama, ameonekana kutotikiswa na mijadala inayozunguka jina lake nje ya uwanja, akisisitiza kuwa mambo hayo hayana nafasi katika maisha yake ya soka.

Chama ameyasema hayo jana wakati wa tukio la Simba Media Day lililofanyika katika Uwanja wa MO Arena, Bunju jijini Dar es Salaam, huku kauli yake ikija wakati ambapo kumekuwa na mjadala mkubwa mitandaoni kuhusu uhusiano wake na klabu yake ya zamani, Yanga SC.

Nyota huyo wa Zambia amesema anachagua kuangalia zaidi kile kinachoendelea ndani ya uwanja na majukumu yake kama mchezaji wa Simba, badala ya kuruhusu mijadala ya nje ya uwanja kumvuruga.

"Mimi ni mchezaji mzoefu hayo masuala ya nje ya uwanja hayawezi kunisumbua, akili na mawazo yangu yako kwa klabu ya Simba ambayo mimi na wenzangu tunawajibika katika kuhakikisha tunfikia malengo," alisema Chama

Hivi karibuni Chama alifichua yaliyojiri wakati amesajiliwa na Yanga akiweka wazi kuwa haikuwa dhamira yake kujiunga na timu hiyo lakini mazingira ya wakati huo yalimfanya kuchukua uamuzi ambao ulimfanya asiwe na furaha.

Baada ya kurejea Simba, Chama amerejesha makali yake akiwa sehemu ya wachezaji wanaotegemewa katika kikosi cha Simba, huku mashabiki wakitarajia kuona ubora wake ukionekana zaidi ndani ya uwanja.

More Stories

Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
4h ago
READ MORE β†’
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
7h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
10h ago
READ MORE β†’
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
11h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
14h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
1d ago
READ MORE β†’
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
1d ago
READ MORE β†’
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
1d ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
1d ago
READ MORE β†’