Wapinzani wa Simba Mighty Wonderers wanatarajiwa kuwasili nchini leo kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa utakaopigwa Jumapili.
Mchezo huo wa mkondo wa pili hatua ya awali ya michuano hiyo, utapigwa uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.
Mighty wanatua nchini huku wakiwa tayari wako nyuma kwa bao 1-0 wakipokea kipigo kwenye mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa nchini Malawi.
Wakati timu ikitarajiwa kuwasili leo, Wekundu wa Msimbazi wanaendelea na maandalizi yao Mo Simba Arena kuelekea mchezo huo.
Baada ya ushndi ugenini Simba inahitaji ushindi mwingine au hata matokeo ya sare kwenye mchezo huo ili kutinga raundi ya kwanza.
Kikosi cha kocha Steve Barker kimedhamiria kumaliza kazi mapema pale uwanja wa Uhuru siku ya Jumapili mchezo huo ukitarajiwa kupigwa mbele ya mashabiki wa Simba.
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amewataka mashabiki wa timu hiyo kuendelea kununua tiketi kwa wingi ili kuhakikisha wanaujaza uwanja wa Uhuru siku ya Jumapili.