Mpya

Hatuhitaji kupoteza mchezo dhidi ya Azam Fc - Barker

Mwana Msimbazi By Mwana Msimbazi
β€’
1d ago
Hatuhitaji kupoteza mchezo dhidi ya Azam Fc - Barker

Licha ya muda mchache wa maandalizi, Kocha Mkuu wa Simba Steve Barker amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa kesho Jumatano kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar es salaam.

Akizungumzia maandalizi kuelekea mchezo huo, Barker alisema wamekuwa na muda mfinyu wa maandalizi kutoka mechi iliyopita hata hivyo wanafahamu umuhimu wa mchezo huo.

Barker amesema ili Simba kufikia malengo yake ya msimu huu, mchezo huo ni miongoni mwa mechi ambazo wanahitaji kushinda.

"Tumekuwa na muda mchache wa maandalizi tangu tulipocheza mchezo wa mwisho ila mechi ya kesho ni muhimu sana kwetu."

"Tunahitaji kupata ushindi ili tulinde malengo yetu ya msimu huu. Kama unakumbuka msimu uliopita tulipoteza pointi nne dhidi ya yao."

"Tunataka kuwa bora na kufanya vizuri zaidi msimu huu," alisema Barker

More Stories

Karibu Azam Complex kwenye show za Libasse Gueye
Karibu Azam Complex kwenye show za Libasse Gueye
1h ago
READ MORE β†’
Mzizima Derby; Azam Fc vs Simba leo
Mzizima Derby; Azam Fc vs Simba leo
3h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Jumatano, Septemba 16 2026
Magazeti ya leo Jumatano, Septemba 16 2026
7h ago
READ MORE β†’
Maandalizi ya kuikabili Azam Fc yamekamlika
Maandalizi ya kuikabili Azam Fc yamekamlika
15h ago
READ MORE β†’
Mzizima Derby haijawahi kuwa nyepesi
Mzizima Derby haijawahi kuwa nyepesi
1d ago
READ MORE β†’
Kituo kinachofuata ni MZIZIMA DERBY
Kituo kinachofuata ni MZIZIMA DERBY
1d ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Jumanne, Septemba 15 2026
Magazeti ya leo Jumanne, Septemba 15 2026
1d ago
READ MORE β†’
Doumbia bado kidogo, Mgunda akosha mashabiki
Doumbia bado kidogo, Mgunda akosha mashabiki
1d ago
READ MORE β†’
Tulitaka kutuma ujumbe Afrika - Ahmed
Tulitaka kutuma ujumbe Afrika - Ahmed
1d ago
READ MORE β†’