Transfer

Dirisha la usajili Ulaya linafungwa leo

Joel JJ By Joel JJ
31 Jan 2023
Dirisha la usajili Ulaya linafungwa leo

Dirisha la uhamisho wa Ligi Kuu ya Uingereza litafungwa Jumanne saa 23:00 GMT, michakato mbalimbali ya usajili inatarajiwa kukamilishwa kabla dirisha hilo halijafungwa

Baadhi ya sajili zilizokamilika;

Chelsea wameongeza kasi katika dirisha hili la uhamisho huku wakitafuta njia yao ya kurejea kwenyenafasi ya nne bora. Mmiliki Todd Boehly's Blues wametumia zaidi ya pauni milioni 200 kununua wachezaji saba wapya, akiwemo Benoit Badiashile (£35m), Andrey Santos (£18m), Joao Felix (kwa mkopo na ada ya £9.7m), Noni Madueke (£30.7m) na Mykhailo Mudryk (£62m ikipanda hadi £89m), wengi wao wakiwa na mikataba mirefu.

Kumekuwa na mabadiliko kidogo kutoka kwa vilabu vilivyo juu yao kwenye jedwali, lakini sio sana, huku Liverpool ikimchukua mshambuliaji wa Uholanzi Cody Gakpo kutoka PSV, Arsenal ikimsajili Leandro Trossard kutoka Brighton na Newcastle ikitumia pauni milioni 45 kumpata Anthony Gordon kutoka Everton.

Kumekuwa na ujio wa kuvutia Manchester United, huku mshambuliaji wa Uholanzi Wout Weghorst akijiunga kwa mkopo kutoka Burnley.

kumekuwa shughuli nyingi miongoni mwa vilabu ambavyo changamoto kuu msimu huu ni kusalia kwenye ligi. Wolves imekuwa na shughuli nyingi, ikiwasajili washambuliaji Matheus Cunha na Pablo Sarabia, kiungo Mario Lemina na beki Craig Dawson ili kuongeza kikosi cha Julen Lopetegui.

Nottingham Forest haijapunguza kasi yake baada ya majira ya kiangazi ambapo walisajili wachezaji 23, huku viungo wa kati wa Brazil Danilo na Gustavo Scarpa, na mshambuliaji Chris Wood, wakihamia City Ground mwezi huu.

Leeds walivunja rekodi yao ya usajili kwa kumsajili mshambuliaji Georginio Rutter na pia wamekubali dili la kumnunua kiungo wa kati wa Marekani Weston McKennie kutoka Juventus kwa mkopo wa awali, wakati Bournemouth (Dango Ouattara kwa £20m), West Ham (Danny Ings kwa £12m) na Southampton (Mislav Orsic na Carlos Alcaraz kwa jumla ya £20m) wamehama.

Limekuwa dirisha gumu lauhamisho kwa Everton, ambao walimpoteza Gordon aliyetajwa hapo awali na kumuona Arnaut Danjuma akiwapa kisogo kabla ya kusajiliwa na Spurs muda mfupi baada ya kumfukuza meneja Frank Lampard.

Kiungo wa kati wa Stuttgart Naouirou Ahamada anafanyiwa uchunguzi wa kimatibabu kabla ya uhamisho wa euro 11m (£9.7m) kwenda Crystal Palace, wakati kiungo wa Newcastle Jonjo Shelvey anazungumza na Nottingham Forest kuhusu uhamisho ambao utamfanya kuwa mchezaji wa 26 kusajiliwa msimu huu.

Wachezaji kadhaa pia wamehusishwa na uhamisho wa Ligi Kuu, kama vile mshambuliaji wa Coventry Viktor Gyokeres, beki wa Stoke Harry Souttar na kiungo wa Sheffield United Sander Berge.

BBC

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
6h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
7h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
9h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
9h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
10h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
10h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
11h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
11h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
11h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
13h ago
READ MORE →