Simba - Singida

Simba yaifumua Singida BS 3-1

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Feb 2023
Simba yaifumua Singida BS 3-1

Mnyama ameunguruma dimba la Mkapa leo akiifumua Singida Big Stars mabao 3-1 katika mchezo wa ligi kuu ya NBC

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira ameanza kujibu maswali ya Wanasimba kuhusiana na mbinu zake leo wakishuhudia kandanda safi kutoka kwa timu yao

Simba ilionyesha kuhitaji ushindi tangu dakika ya kwanza, na iliwachukua dakika nane tu kufungua ukurasa wa mabao kupitia kwa Jean Baleke

Ikiwa ni mechi yake ya pili kwenye ligi, Baleke amefunga bao lake la pili, usajili bora unaoilipa Simba mapemaaa

Ilikuwa mpira wa adhabu kutoka kwa Chama uliotua kwenye guu la kushoto la Baleke na bila ajizi akaifungia Simba bao la kuongoza

Chama hakuwa amemaliza kutoa assist katika mchezo huo kwani dakika chache baadae akajaza mtungi mwingine kupitia mpira wa adhabu ambao safari hii ulijazwa kimiani na Saido Ntibazonkiza

Bao la 10 kwa Ntibazonkiza msimu huu, likiwa ni bao lake la sita tangu atue Simba

Bruno Gomez akaifungia Singida BS bao pekee kupitia mpira wa adhabu kabla ya timu hizo kwena mapumziko Simba ikiwa mbele kwa mabao 2-1

Kipindi cha pili Simba ilirejea na kasi ileile waliyomaliza nayo na hakuwa mwingine bali yule fundi wa mabao ya CAF, Pape Ousmane Sakho

Ilikuwa dakika ya 58 Sakho alifunga bao kama alilowafunga Asec Mimosas kwenye michuano ya CAF msimu uliopita na kushinda tuzo ya bao bora la CAF

Ni vilevile, safari hii akiitendea haki krosi ya Shomari Kapombe kutoka upande wa kulia

Ni alama tatu muhimu kwa Simba ambazo kwa hakika zimeendelea kuiweka Simba kwenye nafasi nzuri katika mbio za ubingwa

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
9h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
9h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
13h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
16h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
17h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
17h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
18h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’