Vinara wa Ligi Kuu ya NBC, Yanga leo watakuwa na nafasi ya kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi pale watakapoikabili Namungo Fc katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Yanga itahitaji kushinda mchezo huo ili kurudisha gap la pointi dhidi ya watani zao Simba kuwa sita
Jana Simba ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Singida BS na hivyo kufikisha alama 53 wakati Yanga ikiwa kileleni na alama 56
Mchezo kati ya Yanga dhidi ya Namungo Fc haujawahi kuwa mwepesi, pamoja na Yanga kushinda mechi mbili za mwisho zilizokutanisha timu hizo
Katika misimu mitatu iliyopita, Yanga imeshinda mara mbili tu dhidi ya Namungo katika ligi kuu
Hivyo utakuwa mchezo mgumu ambao hakuna shaka utawapa burudani mashabiki wa soka nchini
Tangu ujio wa kocha Denis Kitambi, Namungo Fc wameimarika wakishika nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi wakiwa na alama 27
Pengine leo watahitaji kushinda mechi hiyo ngumu ili kuendelea kusogea nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi
Namungo Fc wametolewa kwenye michuano ya kombe la FA hivyo kama watahitaji kushiriki Kimataifa msimu ujao, basi wanahitaji kumaliza katika nafasi tatu za juu