Timu ya Taifa ya Senegal usiku wa kuamkia leo ilifanikiwa kutwaa taji la Michuano ya CHAN baada ya kuichapa Algeria kwa mikwaju wa penati 5-4 kufuatia matokeo ya suluhu ya bila kufungana
Algeria wenyeji wa michuano hiyo inayoshirikisha wachezaji wanaocheza soka la ndani, itabidi wailaumu wenyewe kwa kushindwa kutumia vyema nafasi nyingi walizotengeneza
Senegal sasa wanashikilia mataji yote mawili ya Mataifa barani Afrika kwani pia ndio mabingwa wa michuno ya AFCON



