Beki wa kati wa England Harry Maguire, 29, na kiungo wa kati wa Scotland Scott McTominay, 26, wataongoza uhamisho wa wachezaji sita wenye majina makubwa Manchester United msimu huu.(The Mirror)
West Ham wana uhakika wa kupata ada ya uhamisho wa zaidi ya pauni milioni 80 kwa kiungo wa kati wa England Declan Rice, huku Newcastle wakitarajiwa kuungana na Arsenal na Chelsea katika mbio za kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24.(Football Insider)
Barcelona, Atletico Madrid na AC Milan zote zimefanya uchunguzi kuhusu mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 33, kufuatia kukosekana kwenye kikosi cha Chelsea cha Ligi ya Mabingwa(Mail) Chelsea wako tayari kupambana na Manchester United kumnunua mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 24(Mirror)
Madrid "wameweka nia yao" kumsaini mlinzi wa Wolverhampton Wanderers ya Uhispania Hugo Bueno, 20. (AS via Sport Witness)
West Ham wana uhakika wa kupata ada ya uhamisho wa zaidi ya pauni milioni 80 kwa kiungo wa kati wa England Declan Rice, huku Newcastle wakitarajiwa kuungana na Arsenal na Chelsea katika mbio za kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24.(Football Insider)
Atletico Madrid na AC Milan zote zimefanya uchunguzi kuhusu mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 33, kufuatia kukosekana kwenye kikosi cha Chelsea cha Ligi ya Mabingwa(Mail)
Chelsea wako tayari kupambana na Manchester United kumnunua mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 24(Mirror) Atletico Madrid "wameweka nia yao" kumsaini mlinzi wa Wolverhampton Wanderers ya Uhispania Hugo Bueno, 20. (AS via Sport Witness).
Arsenal na Tottenham ni miongoni mwa vilabu ambavyo vimeonyesha nia ya kumnunua mshambuliaji wa Barcelona Mhispania Ansu Fati, lakini Bayern Munich wanatajwa kumtaka zaidi mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)
The Gunners, wakati huohuo, watakuwa wanapewa nafasi kubwa ya kumsajili kiungo wa kati wa Leicester City na Ubelgiji Youri Tielemans, 25, msimu wa joto. (TeamTalk)
Tottenham inaweza kuripotiwa kutumia uhusiano mzuri na Atletico Madrid kuwasajili winga wa Ubelgiji Yannick Carrasco, 29, na kipa wa Slovenia Jan Oblak, 30, katika dirisha lijalo la usajili.(Mail)
Real Madrid walipewa nafasi ya kumsajili beki wa pembeni wa Ureno Joao Cancelo, 28, kutoka Manchester City, lakini klabu hiyo ya Uhispania iliamua kutoendelea na mpango huo kwa vile wanafuraha na kikosi cha sasa. (Fabrizio Romano kupitia Twitter)
Kiungo wa kati wa Uhispania Isco, 30, anaripotiwa kusubiri pendekezo madhubuti kwa maajenti wake kutoka Everton huku akiendelea kutafuta klabu mpya baada ya mkataba wake na Sevilla kuvunjwa. (TuttoJuve - kwa Kiitaliano)
BBC