Mbio za ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza zinaendelea kubaki salama kwa Arsenal baada ya wapinzani wao wa karibu Manchester City kuangukia pua kwa kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Tottenham Hotspurs
Ikumbukwe Arsenal walichapwa bao 1-0 dhidi ya Everton katika mechi yao iliyopita hivyo kama Man City angepata ushindi dhidi ya Spurs, wangepunguza gap la pointi kutoka tano kubaki mbili
Lakini sasa Arsenal wanaendelea kubaki kileleni kwa tofauti ya alama tano huku pia wakiwa na mchezo mmoja mkononi
Hata hivyo Arsenal na Manchester City bado hazijacheza mechi zao mbili za ligi
Mechi ya duru ya kwanza haikupigwa mpaka sasa tangu ilipoahirishwa baada ya kifo cha Malkia Elizabeth
Pengine hizi ndio mechi ambazo zitawapa uhakika Arsenal kama msimu huu watashangilia ubingwa baada ya miaka 19 au la
Ushindi wa Spurs unawafanya wasogee karibu na nne bora wakifikisha alama 39, alama moja nyuma ya Newcastle United yenye alama 40