Nyota wa Ghana Christian Atsu ambaye alikuwa haonekani baada ya kutokea kwa tetemeko la ardhi nchini Uturuki amepatikana akiwa hai
Ni baada ya juhudi za ukoaji kufanyika. Atsu amepelekwa hospitali kwa matibabu zaidi akipata majeraha kwenye mguu wake wa kulia na pia anasumbuliwa na matatizo ya kupumua.
Pia mkurugenzi wa ufundi wa klabu ya Hatayaspor ambayo Atsu anaitumikia, Tamer Savut nae amepatikana akiwa hai.
Atsu ni mchezaji wa timu ya Taifa ya Ghana akiwa pia amewahi kuzitumikia klabu za Chelsea na Newcastle United zinazoshiriki ligi kuu ya Uingereza



