Tetesi za soka Ulaya, Jumanne, Februari 07 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th February 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumanne, Februari 07 2023

Paris St-Germain wanataka kumsajili kiungo wa kati wa Ureno Bernardo Silva, 28, ambaye yuko tayari kuondoka Manchester City, lakini inaweza kukabiliana na ushindani kutoka kwa Barcelona. (Le10 Sport)

Manchester United itajaribu kuwauza mshambuliaji wa Ufaransa Anthony Martial, 27, beki wa kati wa England Harry Maguire, 29, na beki wa kushoto wa Brazil Alex Telles, 30, katika msimu wa joto huku klabu hiyo ikilenga kutoa nafasi kwa mshambuliaji mpya kutoka klabu ya Tottenham nahodha wa Uingereza. Harry Kane 29, au mchezaji wa kimataifa wa Napoli mwenye umri wa miaka 24 Victor Osimhen.

Tottenham haitamuuza mfungaji bora wa klabu Kane kwa klabu pinzani msimu huu wa joto. (Times)

Manchester United itahitajika kulipa pauni milioni 120 kumnunua kiungo wa kati wa England Declan Rice, 24, kutoka West Ham, baada ya dau la pauni milioni 100 kukataliwa msimu uliopita. (TalkSport)

Carlos Corberan wa West Brom anaongoza kwenye orodha fupi ya Leeds ya kocha wa kuchukua nafasi ya Jesse Marsch aliyetimuliwa. (Guardian)

Real Madrid wanaamini kuwa kiungo wa kati wa Uingereza Jude Bellingham, 19, atachagua kuhamia ligi kuu England atakapoondoka Borussia Dortmund. (Athletic)

Wamiliki wa Southampton walijadili mustakabali wa meneja Nathan Jones baada ya timu hiyo kuchapwa 3-0 Jumamosi na Brentford lakini wanatazamiwa kuendelea kubaki naye kwa sasa. (Sport)

Jones anatarajiwa kuiongoza timu hiyo katika mechi ya nyumbani ya Southampton dhidi ya Wolves Jumamosi. (90Min)

Meneja wa zamani wa Southampton Ralph Hasenhuttl anaongoza mbio za kuwa meneja mpya wa klabu ya Ujerumani ya Hoffenheim baada ya klabu hiyo kumtimua Andre Breitenreiter. (Sky Sports)

Chelsea wanamfuatilia mlinda mlango wa Porto na Ureno Diogo Costa, 23, huku wakitarajia kushughulikia mustakabali wa mlinda mlango wao katika majira ya joto. (90Min)

Inter Milan wamemuongeza mlinzi wa Fulham Tosin Adarabioyo, 25, kwenye orodha ya nyota inayowasaka kuchukua nafasi ya mlinzi wa kati wa Slovakia Milan Skriniar, 27, ambaye anatarajiwa kuondoka katika kikosi hicho cha Serie A mkataba wake utakapokamilika msimu wa joto. (Tuttomercatoweb)

Kocha wa zamani wa Newcastle United, Steve Bruce, alikataa nafasi ya kuifundisha klabu yake ya zamani ya Wigan Athletic baada ya timu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza kumuomba achukua nafasi ya kocha Kolo Toure aliyetimuliwa hivi majuzi. (Football Insider)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.