Simba yazindua jezi za CAF

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th February 2023


Simba yazindua jezi za CAF

Klabu ya Simba imezindua jezi rasmi ambazo zitatumika katika mechi za hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Simba imeingia makubaliano na Bodi ya Utalii kuitangaza nchi kupitia nembo ya VISIT TANZANIA

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa jezi hizo, Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally alisema M-Bet itaendelea kuwa Mdhamini Mkuu wa Simba katika michuano ya ligi ya mabingwa

Simba itavaa jezi zenye nembo ya VISIT TANZANIA katika mechi tu lakini inaposafiri itaendelea kuvaa jezi za Mdhamini Mkuu, M-Bet

Jezi mpya zitaanza kuuzwa rasmi Februari 15 na zitapatikana kwa Tsh 35,000/-


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.