Mchezo wa kwanza kwa Simba kundi C ligi ya mabingwa dhidi ya Horoya Ac umemalizika kwa wenyeji kuibuka na ushindi wa bao 1-0
Ulikuwa mchezo uliokuwa wazi, pengine Simba itajilaumu kwa kutotumia nafasi walizotengeneza hasa kwenye kipindi cha pili
Nahodha John Bocco, Clatous Chama walipoteza nafasi adimu ambazo pengine zingebadili matokeo hayo
Mlinda lango Aishi Manula ameendeleza ubora wake kwenye michuano ya CAF leo akiokoa mkwaju wa penati
Mchezo unaofuata kwa Simba ni nyumbani dhidi ya Raja Casablanca utapigwa Jumamosi ijayo
Hii ni mechi ambayo Simba inazihitaji alama zote tatu
Raja ndio vinara wa kundi C kufuatia ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Vipers Fc katika mchezo wao wa kwanza



