Simba yaanza kwa kipigo Ligi ya Mabingwa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th February 2023


Simba yaanza kwa kipigo Ligi ya Mabingwa

Mchezo wa kwanza kwa Simba kundi C ligi ya mabingwa dhidi ya Horoya Ac umemalizika kwa wenyeji kuibuka na ushindi wa bao 1-0

Ulikuwa mchezo uliokuwa wazi, pengine Simba itajilaumu kwa kutotumia nafasi walizotengeneza hasa kwenye kipindi cha pili

Nahodha John Bocco, Clatous Chama walipoteza nafasi adimu ambazo pengine zingebadili matokeo hayo

Mlinda lango Aishi Manula ameendeleza ubora wake kwenye michuano ya CAF leo akiokoa mkwaju wa penati

Mchezo unaofuata kwa Simba ni nyumbani dhidi ya Raja Casablanca utapigwa Jumamosi ijayo

Hii ni mechi ambayo Simba inazihitaji alama zote tatu

Raja ndio vinara wa kundi C kufuatia ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Vipers Fc katika mchezo wao wa kwanza


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.