Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya US Monastir ambao utapigwa kesho Jumapili jijini Tunis
Aidha Nabi ameupongeza uongozi wa Yanga kwa kuipeleka timu mapema Tunisia, wamekuwa na muda mzuri wa kufanya maandalizi pamoja na kuzoea hali ya hewa
Nabi amesema wanakwenda kupambana na timu nzuri inayocheza soka la ushindi
"Nawashukuru viongozi wa Yanga kwa kuifikisha timu huku mapema kwa sababu ya hali ya hewa. Tumejiandaa vizuri, wachezaji wana ari kubwa"
"US Monastir ni timu ambayo inatoka sehemu nilipozaliwa, ni timu nzuri yenye upinzani lakini tumejiandaa vizuri, tutapambana kwa pamoja ili kupata matokeo mazuri," alisema Nabi
Nae mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele amesema wanajua wanakwenda kupambana na timu nzuri, wachezaji wako tayari
"Sisi kama wachezaji tumejiandaa vizuri na tunajua tunakwenda kukutana na timu nzuri. Tupo tayari, tumekuja hapa kupambana, tutapambana mpaka mwisho"