Timu ya Ihefu Fc inayosjiriki Ligi Kuu ya NBC imemtangaza John Simkoko kuwa kuwa kocha mkuu wa timu hiyo kuanzia leo Februari 12, 2023.
Simkoko amechukua nafasi ya Juma Mwambusi aliyeachana na timu hiyo baada ya kuitumikia kwa miezi miwili tu.
Taarifa ya Ihefu imeeleza kuwa Simkoko ataungana na benchi la ufundi ili kufanikisha malengo yao.
Kabla ya utambulisho wa Simkoko, Ihefu ilikuwa chini ya Kocha Zuberi Katwila ambaye amekuwa na timu hiyo kwa muda mrefu
Ihefu Fc leo wanacheza na Singida Big Stars katika mchezo wa ligi kuu ya NBC



