Yanga

Yanga dimbani dhidi ya US Monastir

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Feb 2023
Yanga dimbani dhidi ya US Monastir

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika, Yanga leo wanashuka uwanja wa Olympique Hammadi Agrebi huko Tunisia kumenyana na US Monastir

Ni mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ambao utapigwa saa 1 usiku

Yanga itaingia kwenye mchezo huo ikiwa na kumbukumbu nzuri kunako uwanja wa Olympique Hammadi Agrebi kwani ni katika uwanja huo walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Club Africain na kutinga hatua ya makundi

Katika mchezo huo Yanga inahitaji kushinda lakini hata matokeo ya sare yatakuwa muhimu sana kwa Wananchi

Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amesema malengo yao katika michuano hiyo ni kutinga robo fainali hivyo leo wanahitaji kushinda au sare

Hersi alisema wana mkakati kabambe wa kuhakikisha wanashinda mechi zao tatu watakazocheza nyumbani na ugenini kuvuna angalau alama mbili

Kazi ya kusaka alama za ugenini wanaianza leo mbele ya Monastir ambayo imekuwa na msimu mzuri kwenye ligi ya Tunisia

Monastir ni vinara wa kundi A katika ligi ya Tunisia ambayo timu ziko katika makundi mawili

Lakini pia ikumbukwe Monastir ndio waliwaondosha mashindanoni mabingwa watetezi wa kombe la Shirikisho RS Berkane

Hivyo ni wazi utakuwa mchezo mgumu wenye upinzani mkali

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
43m ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
56m ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
1h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
4h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
8h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
9h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
10h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
11h ago
READ MORE β†’