PSG wameshindwa kutamba nyumbani kwenye mchezo wa kwanza hatua ya 16 bora michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya wakikubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Bayern Munich
Kingsley Coman ndiye aliyepeleka msiba PSG akifunga bao pekee la Bayern Munich katika ushindi huo muhimu wa bao 1-0 ugenini
Koeman ni mzaliwa wa Paris na kukulia PSG, Coman alifunga bao pekee wakati Bayern ilipoilaza timu ya Ufaransa kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa 2020 na akawa mfungaji pekee mabingwa hao wa Ujerumani walipotinga hatua ya robo fainali
Ni mechi ya tatu mfululizo PSG wanapoteza katika mashindano yote na sasa watakuwa na kazi ya ziada kwenye kusaka ushindi ugenini kule Munich
Katika mchezo mwingine uliopigwa jana, Ac Milan walianza vyema nyumbani kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tottenham Hotspurs
Ac Milan walifunga bao pekee mapema tu kwenye dakika ya saba kupitia kwa Diaz katika mchezo ambao ulishuhudiwa na zaidi ya mashabiki 74,000
Pamoja na kupoteza mchezo huo Spurs inayonolewa na Antonio Conte ilicheza vyema hasa katika eneo la kiungo ambapo nyota wa Senegal Sarr mwenye umri wa miaka 20 alin'gara
Timu hizo zitarudiana baada ya wiki mbili nchini Uingereza



