Manchester City wamefufua uoya nia yao ya kumnunua kiungo wa kati wa West Ham na England Declan Rice, 24. (90Min)
Liverpool wanashinikiza kumsajili kiungo wa kati wa England Mason Mount, 24 ambaye mazungumzo yake ya kuongeza kandarasi yake Chelsea yakisuasua (Mail)
Inter Miami ya David Beckham iko katika nafasi nzuri ya kumsajili mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi, 35, iwapo ataamua kuondoka Paris St-Germain. (Mirror)
Lakini baba yake na Messi ambaye ni wakala wake pia, Jorge Messi, anasema hakuna uwezekano wa mchezaji huyo kurejea klabu yake ya zamani ya Barcelona tena. (ESPN)
Aston Villa wana nia ya kutaka kumnunua mshambuliaji wa Roma Muingereza Tammy Abraham, 25. (90min)
Leeds United wanaongoza katika mbio za kumsajili winga wa Canada Tajon Buchanan, 24, kutoka Club Bruges. (Calciomercato, via TeamTalk)
Chelsea bado hawajatuma maombi ya kibali cha kufanya kazi kwa ajili ya kiungo wake mpya wa kati wa Brazil Andrey Santos, 18, ambaye walimsajili mwezi Januari. (Athletic)
Juventus wameamua kumuuza kiungo wa kati wa Sweden Denis Zakaria mwenye umri wa miaka 26 akimaliza mmkopo wake Chelsea. (Standard)
Leeds wamemwambia bosi wao wa muda Michael Skubala, 40, kuwa anaweza kusalia kuinoa hadi mwisho wa msimu. (Min 90)
Newcastle United wanajiandaa kumpa mlinzi wa Uingereza Dan Burn, 30, mkataba mpya. (Football Insider)
Meneja wa Everton Sean Dyche anapanga kuangalia mtindo mzima wa maisha wa mshambuliaji wa England Dominic Calvert-Lewin, ikiwa ni pamoja na godoro analolalia, anapojaribu kukabiliana na masuala ya uimara wa kimazoezi na afya ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Times)
BBC