Rais wa Yanga Injinia Hersi Said leo alikuwa miongoni mwa viongozi waandamizi wa klabu hiyo walioshiriki jogging iliyoanzia Makao Makuu ya Yanga, Jangwani jijini Dar es salaam
Ni sehemu ya hamasa kuelekea mchezo wa kombe la Shirikisho ambao Yanga watacheza na TP Mazembe siku ya kesho Jumapili katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Mtendaji Mkuu wa Yanga Andrew Mtine, Mkurigenzi wa Mashabiki na Wanachama Haji Mfikirwa, Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Ali Kamwe ni miongoni mwa viongozi wengine wa Yanga walioshiriki jogging hiyo




