Mwili wa nyota wa Ghana Christian Atsu umepatikana chini ya jengo alilokuwa akiishi kusini mwa Uturuki baada ya tetemeko kubwa la ardhi wiki iliyopita
Wakala wa mchezaji huyo amethibitisha kupatikana kwa mwili wa nyota huyo wa zamani klabu za Chelsea na Newcastle United
"Mwili wa Atsu ulipatikana chini ya vifusi," Murat Uzunmehmet aliwaambia waandishi wa habari huko Hatay, ambapo mwili wa mwanasoka huyo umepatikana
"Kwa sasa, vitu zaidi bado vinatolewa. Simu yake pia ilipatikana"
Atsu aliahirisha safari yake kwenda Ufaransa saa chache kabla ya tetemeko hilo. Mghana huyo aliamua kusalia na klabu hiyo baada ya kufunga bao la kufutia machozi katika mechi ya Februari 5 ya Super Lig
Awali ilitolewa taarifa ya Atsu kupatikana akiwa hai lakini klabu yake ilikanusha
Zaidi ya watu 35,000 wamepoteza maisha katika tetemeko la ardhi lililozikumba nchi za Syria na Uturuki