Sheikh Jassim bin Hamad Al Thani, Mwenyekiti wa benki moja kubwa ya Qatar, amethibitisha kuwa taasisi yake itawasilisha ombi la kuinunua klabu ya Manchester United.
Aidha, kulingana na BBC Ineos, inayomilikiwa na Sir Jim Ratcliffe, pia imetuma ofa rasmi kutaka kuinunua Man United
Bilionea Ratcliffe alikuwa tayari ameeleza nia yake ya kuinunua United baada ya familia ya Glazer, iliyoinunua United mwaka 2005, kuweka wazi mpango wa kuiuza klabu hiyo
Muungano wa Qatar wa Sheikh Jassim ulisema kuwa wamepanga kuirudisha United kwenye hadhi yake ya zamani
Matajiri hao kutoka Qatar wanataka kuwekeza katika timu za mpira wa miguu, kituo cha mazoezi, uwanja na miundombinu, uzoefu wa mashabiki na jamii inayounga mkono klabu
"Maono ya zabuni ni Manchester United kujulikana kwa ubora wa soka, na kuonekana kama klabu kubwa zaidi ya soka duniani," ilisema taarifa ya Sheikh Jassim