Yanga

Nabi afunguka maandalizi ya Yanga mechi ya Mazembe

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Feb 2023
Nabi afunguka maandalizi ya Yanga mechi ya Mazembe

Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya TP Mazembe ambao utapigwa kesho Jumapili katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Akizungumza katika mkutano na Wanahabari, Nabi amesema baada ya kupoteza mchezo dhidi ya US Monastir, wamefanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza katika mchezo huo na sasa wako tayari kuikabili Mazembe

Nabi amewaomba radhi Mashabiki na Wanachama wa Yanga kutokana na matokeo hayo ambayo waliyapata baada ya kufanya makosa

"Tunawaomba radhi Mashabiki na Wanachama wetu kwa kupoteza mchezo dhidi ya Monastir. Yalikuwa makosa yetu lakini tumepata muda wa kufanyia kazi mapungufu yote na sasa tuko tayari kwa mchezo unaofuata dhidi ya TP Mazembe"

"Mashindano haya hayamaliziki kwa mechi moja hivyo bado tunayo nafasi ya kufanya vizuri katika mechi zote zinazofuata"

"Morali ya wachezaji iko juu, wanajituma mazoezini na kuonyesha wanataka kushinda mchezo dhidi ya TP Mazembe. Hali hiyo inanipa matumaini kuona tutakuwa na mchezo mzuri hapo kesho," alisema Nabib

Nabi amebainisha kuwa katika mchezo huo atawakosa wachezaji wawili Bernard Morrison ambaye ni majeruhi na Salum Abubakar 'Sure Boy' ambaye anauguliwa na mtoto

Aidha Nabi amesema kiungo mshambuliaji Stephane Aziz Ki atafanyiwa tathmini baada ya mazoezi ya mwisho leo kuona utayari wake akiwa amekosa mazoezi kwa siku mbili kutokana na matatizo ya kifamilia

Nabi pia alijibu maswali ya wanahabari waliowaulizia wachezaji Mamadou Doumbia na Feisal Salum 'Fei Toto'

Nabi amesema Doumbia anaendelea kufanya mazoezi na wachezaji wenzake na sababu pekee inayomfanya hachezi kwa sasa ni kwa kuwa hana muunganiko na wenzake wakati suala la Feisal amesema sio kipaumbele kwa sasa kwa sababu kwa muda wote ambao amekosekana wachezaji wengine wametekeleza vyema majukumu yao

"Feisal ni mchezaji mzuri, tunafahamu bado ana mkataba na Yanga hivyo akirudi tutamkaribisha kwa mikono miwili lakini hata asiporudi sio kwamba Yanga haitaendelea"

"Wachezaji na makocha wanapita lakini Yanga itaendelea kubaki. Katika mwezi mmoja ambao amekosekana sisi benchi la ufundi tulitengeneza timu kwa kuzingatia wachezaji tulionao"

"Focus yetu kwa sasa ni mchezo dhidi ya TP Mazembe ambao tunahitaji kushinda," alisema Nabi

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
2h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
6h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
6h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
7h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
8h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
8h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
9h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
9h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’