Kuna mwenye swali?. Ushindi mnono wa mabao 3-1 wameupata Yanga dhidi ya TP Mazembe katika mchezo wa kombe la Shirikisho uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Wakiwa katika ubora wa hali ya juu, vijana wa Kocha Nasreddine Nabi walihitaji dakika 11 kufunga mabao mawili kupitia kwa Mudathir Yahya na Kennedy Musonda
Yanga ilitawala mchezo kwa muda mwingi kwenye kipindi cha kwanza huku TP Mazembe wakirejea wakiwa bora zaidi katika kipindi cha pili
Hata hivyo leo safu ya ulinzi ya Yanga ilikuwa bora sana chini ya nahodha Bakari Nondo Mwamnyeto. Bao pekee la Mazembe lilifungwa na Alex Ngonga kupitia mpira wa adhabu
Wakati Mazembe wakitafuta bao la kusawazisha kwenye dakika za majeruhi, Tuisila Kisinda akamaliza shughuli akifunga bao mahiri baada ya pasi kutoka kwa Mayele
Ni alama tatu muhimu kwa Yanga ambazo zinawapeleka mpaka nafasi ya tatu kwenye msimamo wa kundi D huku Wananchi wakiondoka na milioni 15 za Mama na milioni 3 za RC wa Mtwara



