Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema leo watachukua tahadhari kubwa katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya KMC ambao utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Kamwe amesema wanatambua ubora wa KMC licha ya nafasi waliyopo kwenye msimamo wa ligi
"KMC ni timu ngumu na sumbufu mara nyingi kuchukua alama tatu kwa KMC sio rahisi ni lazima kucheza kwa tahadhari kubwa na kujituma"
"Lakini sisi tumetoka kushinda mechi ngumu zaidi ya daraja la juu kwenye soka la Afrika hivyo tutawakabili KMC tukiwa tunajiamini, tunatambua ubora wetu dhidi yao," alisema Kamwe
Kamwe amethibitisha mchezo huo utapigwa saa 10 alasiri akiwataka mashabiki wa Yanga kujitokeza kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa kuishangilia timu yao
"Mchezo utapigwa saa 10 jiioni na sio saa 1 usiku kama ilivyotangazwa awali, mashabiki wetu mje kwa wingi uwanjani kuipa sapoti timu yetu"



