Yanga yazidi kuukaribia ubingwa wa 29

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd February 2023


Yanga yazidi kuukaribia ubingwa wa 29

Yanga imeendelea kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KMC katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Bao la Clement Mzize alilofunga kwenye kipindi cha kwanza lilitosha kuihakikishia Yanga alama tatu muhimu ambazo zimewafanya wafikishe alama 62

Yanga sasa inaongoza ligi kwa tofauti ya alama nane dhidi ya Simba inayoshika nafasi ya pili ikiwa na alama 54 kila timu ikiwa imeshuka dimbani mara 23

Wananchi sasa wanahitaji kushinda mechi tano tu kati ya saba zilizobaki ili kutetea ubingwa wao


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.