Yanga imeendelea kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KMC katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Bao la Clement Mzize alilofunga kwenye kipindi cha kwanza lilitosha kuihakikishia Yanga alama tatu muhimu ambazo zimewafanya wafikishe alama 62
Yanga sasa inaongoza ligi kwa tofauti ya alama nane dhidi ya Simba inayoshika nafasi ya pili ikiwa na alama 54 kila timu ikiwa imeshuka dimbani mara 23
Wananchi sasa wanahitaji kushinda mechi tano tu kati ya saba zilizobaki ili kutetea ubingwa wao








