Yanga safarini Mali

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd February 2023


Yanga safarini Mali

Kikosi cha Yanga kimeondoka jijini Dar es salaam Alfajiri ya leo Alhamisi, Februari 23 kuelekea Mali kwa ajili ya mchezo wa kombe la Shirikisho dhidhi ya Real Bamako ambao utapigwa Jumapili Februari 26

Msafara wa Yanga uliosafiri umejumuisha wachezaji 25, benchi la ufundi na viongozi. Yanga inaelekea Mali wakipitia Ethiopia

Wananchi wanashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa kundi D, wanahitaji ushindi au hata sare ugenini ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga robo fainali


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.