Kikosi cha Yanga kimeondoka jijini Dar es salaam Alfajiri ya leo Alhamisi, Februari 23 kuelekea Mali kwa ajili ya mchezo wa kombe la Shirikisho dhidhi ya Real Bamako ambao utapigwa Jumapili Februari 26
Msafara wa Yanga uliosafiri umejumuisha wachezaji 25, benchi la ufundi na viongozi. Yanga inaelekea Mali wakipitia Ethiopia
Wananchi wanashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa kundi D, wanahitaji ushindi au hata sare ugenini ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kutinga robo fainali




