Mshambuliaji wa Inter Milan, Romelu Lukaku, anaonekana katika hali nzuri zaidi kuliko hapo awali, kwa mujibu wa kocha msaidizi wake wa zamani wa Ubelgiji, Thierry Henry
Lukaku aliingia akitokea benchi dakika ya 58 dhidi ya Porto juzi kabla ya kupachika bao pekee katika ushindi wa mkondo wa kwanza wa hatua ya 16 bora wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Mkurugenzi Mtendaji wa Inter Milan, Beppe Marotta, alikuwa ametilia shaka utimamu wa Lukaku alipoiambia Sky Sport fowadi huyo anahitaji kuwa na umbo kamilifu ili aweze kuwa fiti. Lakini Lukaku, anayecheza kwa mkopo Inter akitokea Chelsea, alitoa majibu kamili alipofunga bao pekee dakika ya 86.
"Nina furaha sana kwa Rom," alisema Henry akiiambia CBS Sports.
"Anaonekana fiti zaidi. Nadhani alikatishwa tamaa hakuanza, jibu pekee unaweza kutoa ni uwanjani, na alifanya hivyo"
Mustakabali wa Lukaku bado haujulikani kwani hadi sasa haujaeleweka wakati wa msimu wake wa mkopo wa muda mrefu akiwa na Inter, akifunga mara nne katika mechi 14.
Hata hivyo, kurejea kwake Chelsea muhula uliopita kulikatisha tamaa vile vile
"Tulikuwa na mazungumzo alipokwenda Chelsea, na nikamwambia atapata ugumu kucheza Chelsea"



