Tuko tayari kuikabili Real Bamako - Nabi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th February 2023


Tuko tayari kuikabili Real Bamako - Nabi

Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Real Bamako ambao utapigwa kesho Jumapili huko Mali

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, Nabi alisema anafahamu ubora wa Real Bamako lakini Yanga imejiandaa vyema, wako tayari kukabiliana nao

"Naifahamu Bamako, ni timu nzuri yenye wachezaji wazoefu, sitegemei utakua mchezo rahisi kwao na kwetu pia, naamini wachezaji wetu wako tayari kupambana kwa dakika 90 za kesho," alisema Nabi

Nabi pia alieleza kuwa na imani na wachezaji wake kuelekea mchezo huu akimtaja mlinda lango Djigui Diarra kama kiongozi atawaongoza wenzake katika mchezo huo hapo kesho

"Diarra ni kipa mzuri mwenye uzoefu mkubwa, ameshathibitisha ubora wake, kuwa naye kwenye kikosi chetu hapa Mali inatupa faida ya kuwa na kiongozi mzuri kwenye safu yetu ya ulinzi"

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, kiungo mshambuliaji Stephane Aziz Ki alisema wamepata maandalizi mazuri kuelekea mchezo huo hivyo wako tayari kuipambania Yanga

"Tunashukuru uongozi kwa kuweka maandalizi mazuri ya kuhakikisha timu inafanya vizuri, sisi kama wachezaji tuko tayari kwa dakika 90 za kesho"


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.