Yanga

Tunayo nafasi ya kufuzu robo fainali - Kaze

Joel JJ By Joel JJ
27 Feb 2023
Tunayo nafasi ya kufuzu robo fainali - Kaze

Kocha Msaidizi wa Yanga Cedric Kaze amesema walikuwa na nafasi ya kushinda mchezo dhidi ya Real Bamako hata hivyo wameridhika na alama moja waliyopata ugenini

Kaze amesema watafanya maandalizi mazuri ili kuhakiisha wanashinda mechi mbili zinazofuata dhidi ya Real Bamako na US Monastir ambazo zitapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

"Tulikuwa na mechi nzuri, wachezaji walipambana kutafuta alama tatu lakini tumefanikiwa kupata alama moja. Haya ni mashindano bado tuna mechi nyingine tatu, mechi mbili tutacheza katika uwanja wa Benjamin Mkapa"

"Sisi benchi la ufundi tutahakikisha tunafanya maandalizi mazuri ili tuweze kushinda lakini tunawaomba mashabiki wetu watupe nguvu zaidi kwa kuja kwa wingi uwanjani katika mechi hizi nyumbani"

"Kwa jinsi kundi lilivyo, tuna nafasi nzuri ya kwenda hatua inayofuata kama tutafanya vizuri katika mechi zilizobaki," alisema Kaze

Mchezo dhidi ya Real Bamako utapigwa Machi 08 na kumalizana nyumbani na US Monastir machi 19

More Stories

Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa uhuru
54m ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
58m ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
1h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
1h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
3h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
13h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
13h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
14h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
17h ago
READ MORE →