Tunayo nafasi ya kufuzu robo fainali - Kaze

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th February 2023


Tunayo nafasi ya kufuzu robo fainali - Kaze

Kocha Msaidizi wa Yanga Cedric Kaze amesema walikuwa na nafasi ya kushinda mchezo dhidi ya Real Bamako hata hivyo wameridhika na alama moja waliyopata ugenini

Kaze amesema watafanya maandalizi mazuri ili kuhakiisha wanashinda mechi mbili zinazofuata dhidi ya Real Bamako na US Monastir ambazo zitapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

"Tulikuwa na mechi nzuri, wachezaji walipambana kutafuta alama tatu lakini tumefanikiwa kupata alama moja. Haya ni mashindano bado tuna mechi nyingine tatu, mechi mbili tutacheza katika uwanja wa Benjamin Mkapa"

"Sisi benchi la ufundi tutahakikisha tunafanya maandalizi mazuri ili tuweze kushinda lakini tunawaomba mashabiki wetu watupe nguvu zaidi kwa kuja kwa wingi uwanjani katika mechi hizi nyumbani"

"Kwa jinsi kundi lilivyo, tuna nafasi nzuri ya kwenda hatua inayofuata kama tutafanya vizuri katika mechi zilizobaki," alisema Kaze

Mchezo dhidi ya Real Bamako utapigwa Machi 08 na kumalizana nyumbani na US Monastir machi 19


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.