Potter akubali lawama Chelsea

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th February 2023


Potter akubali lawama Chelsea

Kocha Mkuu wa Chelsea Graham Potter amekubali lawama kufuatia mwenendo usioridhisha wa klabu ya Chelsea

Jana Chelsea ilikubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Tottenham Hotspurs ikiwa ni mechi ya sita mfululizo Chelsea wanatoka bila ushindi

Aidha katika mechi 15 zilizopita, Chelsea wameshinda mechi mbili tu

Baada ya kipigo kutoka kwa Spurs, Potter anapaswa kuwajibika kwani amepewa kila alichohitaji kutoka kwa mabosi wa klabu hiyo

"Matokeo sio mazuri kwa Chelsea, nabeba lawama kwa matokeo haya. Haya matokeo zio mazuri kabisa na siwezi kuendelea kutegemea utetezi kutoka kwenye Bodi"

"Naamini wachezaji wangu wamefanya kila wanachostahili kufanya lakini hatupati matokeo tunayostahili na hapa ndipo tatizo linapoanzia," alisema Potter

Katika mechi 27 alizoiongoza Chelsea, Potter ameshinda mechi tisa huku akipotea mechi 10 na mechi nane zikiwa sare

Presha ni kubwa huenda Bodi ya Chelsea ikalazimika kufanya mbadiliko katika nafasi yake pamoja na kuwa awali walionyesha kumuunga mkono


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.