Kocha Mkuu wa Chelsea Graham Potter amekubali lawama kufuatia mwenendo usioridhisha wa klabu ya Chelsea
Jana Chelsea ilikubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Tottenham Hotspurs ikiwa ni mechi ya sita mfululizo Chelsea wanatoka bila ushindi
Aidha katika mechi 15 zilizopita, Chelsea wameshinda mechi mbili tu
Baada ya kipigo kutoka kwa Spurs, Potter anapaswa kuwajibika kwani amepewa kila alichohitaji kutoka kwa mabosi wa klabu hiyo
"Matokeo sio mazuri kwa Chelsea, nabeba lawama kwa matokeo haya. Haya matokeo zio mazuri kabisa na siwezi kuendelea kutegemea utetezi kutoka kwenye Bodi"
"Naamini wachezaji wangu wamefanya kila wanachostahili kufanya lakini hatupati matokeo tunayostahili na hapa ndipo tatizo linapoanzia," alisema Potter
Katika mechi 27 alizoiongoza Chelsea, Potter ameshinda mechi tisa huku akipotea mechi 10 na mechi nane zikiwa sare
Presha ni kubwa huenda Bodi ya Chelsea ikalazimika kufanya mbadiliko katika nafasi yake pamoja na kuwa awali walionyesha kumuunga mkono



