Msafara wa kikosi cha Yanga unatarajiwa kuwasili nchini mchana wa leo wakitokea Mali ambako walifanikiwa kupata alama moja muhimu kwenye mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Real Bamako katika mchezo uliomalizika kwa matokeo ya sare ya bao 1-1
Yanga iliondoka Mali jana wakipitia Ethiopia ambako leo wameunganisha ndege ya Dar es salaam
Mabingwa hao wa Tanzania wanashika nafasi ya pili kundi D wakiwa na alama nne nyuma ya vinara US Monastir wenye alama saba kila timu ikiwa imecheza mechi tatu
TP Mazembe wanashinda nafasi ya tatu wakiwa na alama tatu na Real Bamako wakiburuza mkia wakiwa na alama mbili
Yanga ina nafasi nzuri ya kutinga robo fainali kama itashinda mechi mbili zinazofuata dhidi ya Real Bamako na US Monastir ambazo zote zitapigwa uwanja wa benjamin Mkapa



