Rais wa Yanga Injinia Hersi Said amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa motisha kwa klabu za Yanga na Simba ili kuhakikisha zinafanya vizuri katika michuano ta CAF wanayoshiriki
Leo Yanga imekabidhiwa Tsh Milioni 5 baada ya kurejea kutoka Mali ambako walicheza na Real Bamako katika mchezo ambao ulimalizika kwa matokeo ya sare ya bao 1-1
Rais wa nchi Dk Samia anatoa motisha ya Tsh Milioni 5 kwa kila goli ambalo linafungwa kwenye michuano ya ligi ya mabingwa na kombe la Shirikisho
Injinia Hersi amesema motisha hiyo imeongeza morali ya ushindani ndani ya timu akisisitiza kuwa hawatarajii kuacha kitu
"Hii ni ishara nzuri kwetu na kwa wachezaji kupambana kwa ajili ya timu na kupata fedha ambazo ni motisha kwao"
"Matokeo ya sare haukuwa mpango wetu tutahakikisha tunapata pointi tatu, matokeo hayo tumeyaacha Mali sasa tumerudi kujipanga na mechi yetu ya Machi nane ambayo wachezaji wameahidi kupata matokeo ya ushindi ikiwa ni pamoja na kufunga idadi kubwa ya mabao ambayo yatamfanya Rais Samia avunje kibubu zaidi," alisema Hersi
Yanga imefunga mabao manne kwenye hatua ya makundi kombe la Shirikisho na hivyo kukusanya Tsh Milioni 20 wakati watani zao Simba wamefunga bao moja lililowapatia Tsh Milioni 5



