Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amewataka mashabiki wa timu hiyo kuwa tayari kwa mechi mbili za kombe la Shirikisho dhidi ya Real Bamako na US Monastir ambazo zitapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Kamwe amesema hesabu za Yanga kufuzu robo fainali ya michuano hiyo zimenyooka, wanachopaswa kufanya ni kuhakikisha wanashinda mechi hizo za nyumbani ili kufikisha alama 10
Yanga imetangaza kuzindua kampeni ya kuwahamasisha mashabiki kuujaza uwanja wa Benjamin Mkapa katika mchezo dhidi ya Real Bamako ambao utapigwa Jumatano ijayo, March 08 saa 1 usiku
"Tunahitaji nguvu, hamasa na morali ya mashabiki ili kuhakikisha tunashinda mechi hizi. Safari hii tunataka Benjamin Mkapa iwe imefurika mashabiki wote 60,000. Tunakwenda na slogani hii KWA MKAPA NI FULL SHANGWE"
"Mechi hii tumeikabidhi kwa Wanachama na Mashabiki wa Yanga, tunachohitaji ni shangwe la kutosha kutoka kwa mashabiki ili kuwapa hamasa wachezaji wetu zaidi ya vile tulivyofanya katika mchezo dhidi ya TP Mazembe," alisema Kamwe
Kampeni ya hamasa kuelekea mchezo dhidi ya Real Bamako itazinduliwa kesho Alhamisi, Buruguni (Chama) jijini Dar es salaam. Tiketi za mchezo huo zitaanza kuuzwa leo
Viingilio Mzunguuko ni Tsh 3,000/- VIP C ni Tsh 10,000/-, VIP B ni Tsh 15,000/- na VIP A ni Tsh 20,000/-