Kocha ya kupata bao katika mechi 18 mfululizo iwe kufungwa, sare au kushinda, Kocha mkuu wa Singida Big Stars, Hans Van der Pluijm amesema hajafurahishwa na wingi wa mabao yanayopatikana katika kila mchezo
Singida BS tangu mwaka jana Oktoba 18, ilipofungwa 1-0 na Mtibwa Sugar katika Uwanja wa Manungu Complex, timu hiyo imecheza mechi 18 na zote ikifunga bao hata kama inakuwa imepoteza mchezo.
Pluijm ambaye ni kocha wa zamani wa Yanga alisema licha ya kufunga kwenye kila mchezo bado anaamini safu yake ya ushambuliaji ni nzuri hivyo wanatakiwa kufunga mabao mengi zaidi
"Kweli tumefunga kila mchezo tangu tupoteze lakini hainifurahishi sana kama kocha kwa sababu tuna washambuliaji wenye uzoefu wa kutosha kufanya zaidi ya sasa, ushindani wa wachezaji uliopo unachangia nao"
"Tunatengeneza nafasi nyingi zaidi ya mabao ambayo tunafunga, tutaendelea kupambana kuhakikisha tunazifanyia kazi kila nafasi ambazo zinapatikana ndani ya uwanja," alisema Pluijm



