Mabingwa wa Ulaya Real Madrid leo majira ya saa 5 usiku watakuwa wenyeji wa vinara wa La Liga FC Barcelona katika mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya Copa del Rey Uwanja wa Santiago Bernebeu
Michuano hiyo lililoanzishwa mwaka wa 1903, ni mojawapo ya mashindano ya zamani zaidi ya soka ya Hispania
Barcelona inaongoza kwa kutwaa mataji ya Copa del Rey ikishinda mataji 19 waati Real Madrid inashika nafasi ya tatu
Real Madrid na Barcelona zilijikatia tiketi ya kutinga nusu fainali kwa kuzishinda Atletico Madrid na Real Sociedad
Real Madrid ilitinga nusu fainali baada ya kuwachapa majirani zao Atletico Madrid mabao 3-1, wakati Fc Barcelona waliwafunga Real Sociedad 1-0 katika mchezo wa robo fainali
Wakati meneja wa Real Madrid Carlo Ancelotti akitarajiwa kuchezesha kikosi chake kamili, meneja wa Barcelona Xavi Hernandez anaweza kuwakosa baadhi ya wachezaji wake nyota.
Ousmane Dembele na kiungo wa kati wa Barca wa Uhispania Pedri ni majeruhi na hawatakuwa sehemu ya mechi hiyo.
Nyota wa Poland Robert Lewandowski pia huenda akakosekana kutokana na jeraha la misuli ya paja
Pia itakuwa ni mechi ya pili kati ya Real Madrid dhidi ya Barcelona mwaka huu. Katika fainali ya Super Cup 2022-23 mnamo Januari, Barcelona ilishinda Real Madrid 3-1, shukrani kwa mabao ya Gavi, Robert Lewandowski na Pedri.
Mechi nyingine za nusu fainali kwenye Copa del Rey ni kati ya Osasuna dhidi ya Athletic Bilbao.