Simba imetinga robo fainali ya michuano ya kombe la FA kwa ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya African Sports katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru
Katika mchezo huo, kocha mkuu wa Simba Robertinho Oliveira alifanya mabadiliko makubwa ya kikosi chake akiwaweka nje nyota wake muhimu
Hata hivyo tofauti ya uchezaji haikuwa kubwa kwani Simba ilitawala mchezo ikienda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0 lililofungwa na Jean Baleke
Kipindi cha pili Simba iliongeza mabao mengine matatu yaliyofungwa na Kennedy Juma, Mohammed Mussa na Jimmyson Mwanuke
Kutwaa taji la FA ni moja ya malengo ya Simba msimu huu, sasa wametinga nane bora






