FA Cup : Simba yaichapa African Sports 4-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 2nd March 2023


FA Cup : Simba yaichapa African Sports 4-0

Simba imetinga robo fainali ya michuano ya kombe la FA kwa ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya African Sports katika mchezo uliopigwa uwanja wa Uhuru

Katika mchezo huo, kocha mkuu wa Simba Robertinho Oliveira alifanya mabadiliko makubwa ya kikosi chake akiwaweka nje nyota wake muhimu

Hata hivyo tofauti ya uchezaji haikuwa kubwa kwani Simba ilitawala mchezo  ikienda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0 lililofungwa na Jean Baleke

Kipindi cha pili Simba iliongeza mabao mengine matatu yaliyofungwa na Kennedy Juma, Mohammed Mussa na Jimmyson Mwanuke

Kutwaa taji la FA ni moja ya malengo ya Simba msimu huu, sasa wametinga nane bora


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.