Simba wana jambo Coco Beach leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th March 2023


Simba wana jambo Coco Beach leo

Klabu ya Simba imeandaa tukio kubwa kwa Wanachama na Mashabiki wake leo Jumapili kwenye ufukwe wa Coco jijini Dar es salaam

Kuelekea mchezo wao wa ligi ya mabingwa dhidi ya Vipers Fc ambao utapigwa Jumanne, March 07, Wanasimba wanakutana kuweka mikakati ya kuchukua alama zote tatu kwenye mchezo huo

Aidha mashabiki wa timu hiyo wataweza kununua tiketi pamoja na jezi za timu yao maalum kwa michuano ya ligi ya mabingwa (Visit Tanzania)

Meneja wa habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amewataka mashabiki wa timu hiyo kuhudhuria tukio hilo kujenga hamasa kuelekea mchezo wa Jumanne


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.