Bosi wa Liverpool, Jurgen Klopp, amefunguka kuwa, ni lazima wajipange dhidi ya Manchester United kwani kwenye kikosi cha wapinzani wao wana wachezaji wengi bora
Leo Jumapili, Liverpool itavaana na Manchester United katika mchezo wa wa Premier League mzunguko wa pili ukitarajiwa kuchezwa Uwanja wa Anfield
Katika mchezo wa awali ambao Manchester United walikuwa nyumbani Old Trafford, waliibuka na ushindi wa mabao 2-1.
Pamoja na Marcus Rashford kuonekana ndiye mchezaji hatari zaidi ndani ya kikosi cha United, Klopp amesema sio yeye pekee
"Rashford ana uwezo wa kufunga na anafunga mabao rahisi sana, anafanya mambo mazuri uwanjani na anajua namna ya kujilinda. Lakini yeye sio mchezaji pekee wa daraja la juu ndani ya Man United, hivyo tunahitaji umakini mkubwa"
"Kuna mchezaji kama Bruno (Fernandes), napenda namna anavyocheza, akiwa na mpira yupo smati, unaweza kushangaa huyu hapa tu"
"Casemiro na Fred hawa wakichezaji pamoja wanakuwa bora hasa kwa kulinda, kifiziki wako vizuri na wana uwezo wa kufanya mashambulizi ya kushitukiza kama ilivyo kwa Sancho (Jadon) ndiyo maana tunatakiwa kuwa makini na Man United"
"Lakini pia mchezo huu utakuwa mgumu japo wapinzani wetu wanatakiwa kujua matokeo hayahusiani na masuala ya top four, zaidi hapa tunahitaji ushindi," alisema Klopp
Liverpool hawakuwa na mwenendo mzuri msimu huu lakini matokeo ya ushindi dhidi ya Man United leo yatafufua matumaini yao ya kumaliza katika nafasi nne za juu