Manchester United wapigwa kama ngoma Anfield

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th March 2023


Manchester United wapigwa kama ngoma Anfield

Wakitoka kutwaa taji la Carabao, Manchester United wamekutana na kipigo wasichokitarajia kutoka kwa Liverpool wakifungwa mabao 7-0 katika mchezo wa Premia uliopigwa uwanja wa Anfield

Washambuliaji watatu wa Liverpool Cody Gakpo, Mohammed Salah na Darwin Nunez walikuwa mwiba mkali kwa Manchester United kila mmoja akifunga mabao mawili

Roberto Firmino ambaye ametangaza kuondoka Liverpool mwishoni mwa msimu aliingia kuhitimisha kalamu ya mabao kwa Liverpool akifunga bao la saba

Vijana wa Kocha Erick Ten Hag walikuwa na wakati mgumu kwenye mchezo huo mbele ya vijana wa Jurgen Klopp ambao kwa hakika walikuwa wamewaka kwelikweli

Ni ushindi ambao umefufua matumaini ya Liverpool kumaliza kwenye nafasi nne za juu wakiwa nyuma ya Spurs kwa tofauti ya alama tatu tu huku wakiwa na mchezo mmoja mkononi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.