Mshambuliaji wa Ihefu Fc Yacouba Songne ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa ligi kuu ya NBC kwa mwezi February 2023 wakati Kocha Mkuu wa Kagera Sugar ametwaa tuzo hiyo kwa upande wa makocha
Yacouba aliyefunga mabao mawili na kutoa pasi moja ya bao katika mwezi February, aliwashinda Meddie Kagere wa Singida BS na Elias Maguli wa Geita Gold alioingia nao fainali
Kwa upande wa Mexime, aliwashinda Nasreddine Nabi wa Yanga na Fikirini Elias wa Coastal Union

