Taarifa kutoka ndani ya Kagera Sugar zimethibitisha Kuwa kiungo Abdulaziz Makame 'Bui' hajaonekana kambini kwa muda wa miezi miwili na hakuna taarifa yoyote rasmi juu ya alipo mchezaji huyo
Viongozi wa Kagera Sugar walimpa ruhusa ya muda mfupi kwa ajili ya matibabu lakini toka alipoondoka hajarejea na hakuna mawasiliano baina yake na klabu
Taarifa kutoka ndani ya Kagera Sugar zimethibitisha kuwa, uongozi umeamua kusitisha malipo ya stahiki zake kuanzia mwezi huu hadi pale atakapopatikana
Makame alijiunga na Kagera Sugar msimu uliopita akitokea klabu ya Namungo Fc
Kiungo huyo kutoka visiwani Zanzibar pia amewahi kuitumikia klabu ya Yanga