Chelsea kupindua meza dhidi ya Dortmund leo?

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th March 2023


Chelsea kupindua meza dhidi ya Dortmund leo?

Leo Chelsea Fc itakuwa na kazi ngumu ya kupindua matokeo ya mchezo uliopita wakati timu hiyo itakaporudiana na Dortmund katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa utakaopigwa Stanford Bridge.

Mchezo wa raundi ya kwanza, Chelsea ilipoteza bao 1-0 bao la Karim Adeyemi. Ushindi wao dhidi ya Leeds wikiendi iliyopita huenda ukafufua matumaini ya Chelsea kuelekea mchezo wa leo.

Kuelekea mchezo huo, Reece James, Christian Pulisic huenda wakarejea uwanjani, huku beki Thiago Silva atakosekana kutokana na majeraha. Mason Mount atakosekana baada ya kupokea kadi ya njano.

Dortmund, inayoshika nafasi ya pili kwa tofauti ya mabao nyuma ya Bayern Munich kwenye Bundesliga, inasafiri hadi London ikitaka kuandika ushindi wa 11 mfululizo katika michuano yote, huku Chelsea ikitumai kupata ushindi mfululizo kwa mara ya kwanza tangu Oktoba.

Ili kusonga mbele, vijana wa Graham Potter watalazimika kufunga mabao mawili kwenye mechi kwa mara ya kwanza tangu tarehe 27 Disemba.

Chelsea pia wanaingia kwenye kinyang'anyiro hicho wakiwa wametupwa nje ya vikombe viwili vya nyumbani na wako nafasi ya 10 kwenye Ligi ya Kuu

Ligi ya Mabingwa ni fursa yao pekee ya kushinda taji msimu huu Mchezo mwingine wa Ligi ya Mabingwa utakuwa kati ya Benfica dhidi ya Club Brugge, michezo yote itapigwa saa 5 usiku.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.