Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika Simba, leo wametakata uwanja wa Benjamin Mkapa wakiibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Vipers Fc
Bao pekee la ushindi kwa Simba iliyotawala mchezo huo kwa muda mwingi lilifungwa na Clatous Chama kwenye dakika ya 45
Ni ushindi muhimu kwa Simba ambao umewasogeza kwenye nafasi ya pili kundi C baada ya kufikisha alama sita
Wapinzani wao wa karibu Horoya Ac wamekubali kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Raja Casablanca iliyojihakikishia kutinga robo fainali baada ya ushindi huo
Horoya wameshuka nafasi ya tatu katika kundi C wakibaki na alama zao nne
Simba imenusa hatua ya robo fainali kwani sasa inahitaji kushinda mchezo unaofuata dhidi ya Vipers Fc ambao utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa ili kukata tiketi kabla ya mchezo wao wa mwisho dhidi ya Raja Casablanca utakaopigwa huko Morocco




