Simba yanusa robo fainali Ligi ya Mabingwa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th March 2023


Simba yanusa robo fainali Ligi ya Mabingwa

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika Simba, leo wametakata uwanja wa Benjamin Mkapa wakiibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Vipers Fc

Bao pekee la ushindi kwa Simba iliyotawala mchezo huo kwa muda mwingi lilifungwa na Clatous Chama kwenye dakika ya 45

Ni ushindi muhimu kwa Simba ambao umewasogeza kwenye nafasi ya pili kundi C baada ya kufikisha alama sita

Wapinzani wao wa karibu Horoya Ac wamekubali kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Raja Casablanca iliyojihakikishia kutinga robo fainali baada ya ushindi huo

Horoya wameshuka nafasi ya tatu katika kundi C wakibaki na alama zao nne

Simba imenusa hatua ya robo fainali kwani sasa inahitaji kushinda mchezo unaofuata dhidi ya Vipers Fc ambao utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa ili kukata tiketi kabla ya mchezo wao wa mwisho dhidi ya Raja Casablanca utakaopigwa huko Morocco


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.