Afrik Kusini - Ivory Coast

Nyota wawili wafariki uwanjani Ivory Coast, Afrika Kusini

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Mar 2023
Nyota wawili wafariki uwanjani Ivory Coast, Afrika Kusini

Nyota chipukizi wa Ivory Coast, Sylla Moustapha amefariki baada ya kuanguka uwanjani wakati wa mechi ya Ligi Kuu nchini humo kati ya klabu yake, Racing Club d’Abidjan na SOL FC kwenye Uwanja wa Robert Champroux jana.

Moustapha, anayecheza beki amefariki akiwa na umri wa miaka 21. Kupitia ukurasa wa Twitter , Racing Club imeandika

"Mlinzi wetu Sylla Moustapha amefariki jioni hii (Jumapili) baada ya kuugua akiwa uwanjani"

Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Dk Patrice Motsepe ametuma salamu za pole kwa familia ya Sylla Moustapha, Rais wa Shirikisho la Soka la Ivory Coast Idriss Diallo, familia Racing Club d'Abidjan na watu wa Ivory Coast katika kipindi hiki cha majonzi

Huko Afrika Kusini klabu ya DStv Premiership, Richards Bay, jana ilitangaza kufariki kwa mmoja wa wachezaji wao waliocheza dhidi ya Kaizer Chiefs wikendi.

Kiungo wa kati wa klabu hiyo Siphamandla Mtolo, ambaye alikuwa na umri wa miaka 29, anaripotiwa kufariki dunia wakati wa mazoezi ya asubuhi ya klabu hiyo

"Ni kwa huzuni kubwa kutangaza kwamba Klabu ya Soka ya Richards Bay imempoteza mmoja wa viungo, Siphamandla 'Spepe' Mtolo. Alianguka leo asubuhi wakati wa mazoezi," ilisema taarifa ya klabu hiyo.

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
29m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’