Simba

Baleke aiangamiza Mtibwa Sugar

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Mar 2023
Baleke aiangamiza Mtibwa Sugar

Mnyama Simba ameunguruma dimba la Manungu Complex huko Turiani mkoani Morogoro wakiibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa ligi kuu ya NBC

Simba ilihitaji dakika 45 tu kujihakikishia ushindi huku ikihitaji dakika saba tu kufunga mabao mawili ya haraka kupitia kwa Jean Baleke ambaye leo alikuwa shujaa wa Simba baada ya kufunga hat-trik

Akiwa katika kiwango bora, Baleke aliwaweka kwenye wakati mgumu walinzi wa Mtibwa Sugar akiongeza bao la tatu kwenye dakika ya 36 akimalizia mpira wa kichwa kutoka kwa Shomari Kapombe

Baleke amedhihirisha Simba haikufanya makosa kwenda kumsajili kule TP Mazembe. Ametua mwezi Januari na tayari amepachika mabao matano kwenye ligi

Ni ushindi muhimu kwa Simba ambao umewafanya wafikishe alama 57 sasa wakiwa nyuma ya Yanga kwa tofauti ya alama tano

Yanga watacheza na Geita Gold hapo kesho kwenye mchezo utakaopigwa uwanja wa Azam Complex

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
13h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’