Real Madrid yaichapa Espanyol 3-1

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th March 2023


Real Madrid yaichapa Espanyol 3-1

Real Madrid wamepata ushindi wao wa kwanza wa La Liga baada ya mechi tatu walipotoka nyuma na kuifunga Espanyol mabao 3-1

Espanyol walianza vyema Joselu akiwaweka mbele wasumbufu hao kutoka Catalan baada ya dakika nane.

Lakini mabao kutoka kwa Vinicius Jr na Eder Militao yaliipa Real Madrid uongozi na kuhakikisha ushindi kwa bao la dakika za mwisho la Marco Asensio

Real Madrid ambayo iko pointi sita nyuma ya Barcelona iliyoko kileleni huku Real Madrid wakiwa wamecheza mechi moja zaidi, watamenyana na Barca kwenye El Clasico wikendi ijayo.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.