Hatutashuka daraja - Zahera

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th March 2023


Hatutashuka daraja - Zahera

Licha ya kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Dodoma Jiji hapo jana, Kocha Mkuu wa Polisi Tanzania Mwinyi Zahera amesisitiza kuwa haoni timu yake ikiteremka daraja

Polisi Tanzania inashika nafasi ya 16 (mwisho) kwenye msimamo wa ligi wakiwa na alama 19 huku timu hiyo ikiwa imesalia na mechi tano

Zahera amesema anaamini katika mechi zilizosalia bado wana nafasi ya kupambana ili wabaki Ligi Kuu

"Sijafikiria hata siku moja kwamba timu itashuka daraja! Bado zimebaki mechi tano (5) ambazo ni sawa na alama 15"

"Ikifika wakati hata tukishinda alama zitakuwa hazitusaidii kitu tunaweza kuamini tumeshuka lakini kwa sasa bado sifikirii kama hii timu itashuka," alisema Zahera baada ya kipigi cha mabao 2-1 kutoka kwa Dodoma Jiji katika mchezo uliopigwa uwanja wa Jamhuri

Polisi Tanzania wana alama 19, Ruvu Shooting ipo juu yake ikiwa na alama 20. Kwenye eneo la kucheza play offs kuna Coastal Union alama 26 na Tanzania Prisons alama 25 ambazo zinaweza kufikiwa na Polisi Tanzania

Polisi Tanzania inaweza kutoka chini hadi kwenye eneo salama ambalo ni nafasi ya tisa (9) hadi 12 ambako anaweza kuzifikia alama za timu zilizopo eneo hilo

Polisi Tanzania imebakiza mechi dhidi ya Singida Big Stars (A) Ihefu (H), Mtibwa Sugar (H), Azam (A) na Simba (A).


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.