Kocha Mkuu wa Fc Barcelona Xavi Fernandez ameeleza kuvutiwa na kiwango cha kiungo Frank De Jong akieleza timu yake inafurahia huduma yake
De Jong anawindwa na Manchester United tangu dirisha la usajili la majira ya joto hata hivyo kiungo huyo ameweka msimamo hana mpango wa kundoka Fc Barcelona
Kocha wa Manchester United Erik Ten Hag anamuhitaji sana De Jong katika kikosi chake, akiwa mmoja wa wachezaji aliopata nao mafanikio wakati yuko Ajax ambapo msimu wa 2019-20 walitinga nusu fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya
"Frenkie de Jong ni mmoja wa viungo bora zaidi duniani kwa sasa, yuko kwenye kiwango cha kuvutia, anacheza kwa kiwango cha ajabu anatupa mengi, nina furaha sana na Frenkie,"alisema Xavi
Jana De Jong alikuwa sehemu ya kikosi cha Barcelona kilichopata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Athletic Club na kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa La Liga kwa tofauti ya alama tisa dhidi ya wapinzani wao Real Madrid
Fc Barcelona wana alama 65 wakati Real Madrid wana alama 56 timu hizo zikitarajiwa kuchuana katika mchezo wa El Classico mwishoni mwa wiki