Kiungo mshambuliaji wa Simba Clatous Chama 'Mwamba wa Lusaka' ametajwa katika kinyang'anyiro cha wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa wiki wa michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika
Chama ameingia katika kinyan'ganyiro hicho baada ya kuonyesha kiwango bora katika mchezo dhidi ya Vipers Fc uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa March 07
Chama alifunga bao pekee la Simba katika mchezo huo ambao Wekundu wa Msimbazi waliweka hai matumaini ya kufuzu robo fainali wakihitaji kushinda mchezo dhidi ya Horoya AC utakaopigwa March 18
Chama anachuana na Ahmad Zizo wa Zamalek, Peter Shalulile wa Mamelod Sundowns na Walid Sabar wa Raja Casablanca
